Week 17a Review: Juma 17a Tathmini
Loading...
Authors
Alexander, Andy, S.J.
Waldron, Maureen McCann
Issue Date
2000-01-01
Volume
Issue
Type
Text
Language
en_US
Keywords
Alternative Title
Abstract
JUMA LA MARUDIO|Kutua Kwa Muda Ili Kupitia Neema Tulilizopokea|Mwongozo: Neema za Kutuingiza Ndani Zaid|Tunatua tena kidogo ili kutoa nafasi kwa neema tulizopokea kupenyeza ndani zaidi mioyoni mwetu. Tunafanya mafungo haya huku tukiendelea kawaida na maisha na shughuli zetu za kila siku. Sasa tumezizoea sana tafakari zetu za kila siku na tayari zimekuwa zikituletea furaha. Tunajitayarisha kusonga mbele kuelekea kweny tafakari ambazo Yesu atatuonyesha kuhusu safari ya maisha yake.|Juma hili halitupeleki katika maeneo mapya, ila linatuingiza ndani zaidi katika eneo tulilopo. Tunalianza juma hili kwa kuzitazama shauku zetu. Naifanya upya shauku yangu, uchu wangu na uchaguzi wangu kuwa na Yesu—kutaka kumjua kwa ukaribu zaidi, kumpenda kwa undani zaidi na kumfuata kwa moyo zaidi. Juma hili si lenye harakati nyingi ndani moyoni au mawazo makali akilini. Hii ni juma la kufanya uthibitisho. Juma zima, kwa kutumia njia zangu mwenyewe, nakusudia kufanya kumbukumbu ya nia yangu kuu itawale akili na moyo wangu wakati wote, au nafanya bidii katika muda ninaopata kusema tena na tena “Ndiyo, hiki ndicho ninachotafuta; Hiki ndicho ninachochagua—Kuwa nawe Yesu wangu.”
Description
Citation
Publisher
Creighton University, Online Ministries
